Sunday, July 1, 2012

HAPA ZANZIBAR IJIFIKIRIE UPYA.

Zanzibar hata muungano ukivunjika leo haitakuwa na usalama wala Tanganyika haitakuwa na amani naamini hivyo Znzibar. Dhana ya ubaguzi ni dhana endelevu kama ilivyo uhuru usawa, mwanzo wa uhuru wa kitu Fulani ni mwanzo wa madai ya uhuru mwingine tufikirie uhuru uliodaiwa wakati wa uhuru ni uhuru wa zama hizi?
Je wakati tunadai uhuru miaka ya 1950 tulidai uhuru tulidai wa habari, tulipodai usawa ulikuwa usawa wa jinsia, tulipodai umoja ulikuwa wamisikiti au makanisa? Tulipodai umoja ulikuwa wa makanisa? hapa tunaweza kuona kuna dhana pana sana na zinazobadilika kutokana na zama je ni nini lengo. Leo binadam ukiwa na sababu sahihi anaweza kudai apate mabadiliko Fulani kesho aktaka kuwa na mabadiliko hapa ndipo dhana ya ubaguzi na uhuru na usawa zinapofanana ila mwanzo wa kuchoma makanisa umeleta dhana ya kudai kuuvunja muungano. Kwa mtazamo wangu kilichopo nyuma ya pazia ni kuuvunja muungano ili kupata zanzibar itakayokuwa jamhuri ya kiislam.
Nasema hivi kutokana na mfululizo wa matamshi, nani wanataka muungano uvunjike, ,mitazamo yao, misimamo yao, na ‘prediction’ yangu. Ila hata muungano ukivunjika bado ubaguzi hauwezi kuwaishia hapa utaendelea kwasababu ni asili ya ubaguzi kuendelea kawsababu watu hawafanani, hajawahi kufanana, hawatafanana, watatofautina na wataendelea kuwa hivyo.
Waafrika hatugawanywi kwa misingi ya kiafrika ‘dhana za kiafrika, mitazamo ya kiafrika, fikra za kiafrika’ ila kwa misingi wasio waafrika ambazo kama waafrika hatupati faida zaidi ya kutuumiza hivi tunazoamini udini, rangi, mipaka kwa faida ya nani yetu? Ya kiroho? Kwa maisha ya nani yetu na vizazi vya nani? Vyetu? Kila ni nini asili ya chuki tulizonazo sio mawazo yam bongo zetu ni picha tulizojengewa na wao ni tamaduni zao. Huwa najiuliza kwanii zitugawe Waafrika nadhani naweza kupata leo majibu kupitia makala hii.
Kama Afrika inanielewa inatakiwa iwe na uwezo wa kusikia nakutambua kupitia milango yake ya fahamu hivi dhana
Mwanzo wa dai la kuuvunja muungano utazaa kutaka kuivunja pemba na Unguja
TO BE CONTINUED

No comments:

Post a Comment